Hivi karibuni Mariah Carey alizikonga nyoyo za mashabiki huko Angola kwa show ya maana iliyomuingizia kiasi cha dola za Marekani Milioni 1, sawa na bilioni 1 na milioni 600 za kitanzania.
Kundi
la kutetea haki za binadamu ‘Human Right Foundation’ limemkosoa vikali
mwimbaji huyo kwa madai kuwa alikubali kulipwa fedha na binti wa rais wa
Angola Jose Eduardo dos Santos, rais ambaye anatuhumiwa na baadhi ya
makundi ya kutetea haki za binadamu kuwa fisadi.
Mariah
Carey alipiga show ya masaa mawili nchini Angola iliyoandaliwa na Red
Cross ya nchini humo, na kampuni ya simu ya Unitel ambayo inamilikiwa na
binti wa rais Dos Santos aitwae Isabel. Pia Isabel ndiye rais wa Red
Cross nchini Angola.
Rais
wa Human Right Foundation aitwae Thor Halvorssen ameandika tamko
linalomkosoa Mariah Carey, “Mariah Carey haonekani kutosheka na pesa za
dictator, imeripotiwa amelipwa dola milioni 1 kipindi hiki. Miaka mitano
tu iliyopita aliperform kwenye familia ya dictator wa Libya Muammar
Gaddafi.”
0 comments:
Post a Comment